Breaking News

Mkuu wa Mkoa Zanzibar awaposti Alikiba na Diamond


Wakati kukiwa bado fukuto kwa mashabiki mitaani kuhusu ni Ngoma ya Nani kali kati ya Aliyoachia Alikiba 'Seduce Me' na Zilipendwa ya WCB, basi hata serikalini wasanii hao wameendelea kugawagawa viongozi, ambapo Imeonekana Posti hii ya Diamond na Alikiba kwenye ukurasa wa Instagram wa mkuu wa mkoa wa Mjini Magharibi Ayoub Mahmoud iliyoambatana na ujumbe huu

RC Ayoub Mahmoud

"Nimeuelewa sana wimbo wa vijana wetu #wcb wakiongozwa na ndugu @diamondplatnumz hakika nimewaelewa sana kwenye wimbo wao wa #ZILIPENDWA, hii na pia nathamini kazi kubwa iliofanywa na kijana wetu ndugu yangu @officialalikiba, hakika wimbo wako ni wimbo nilio tokea kukubali.


kama kiongozi niko proud sana na kazi nzuri zinazofanywa na vijana wetu kwa kutuwakilisha vyema nje ya mipaka yetu

Ushauri wangu kwenu ni kua,tofauti zenu ziwe za kibiashara na sio vyenginevyo, #seduceme #fire#song

#teammzikimzuri" Aliandika RC Ayoub

Mpaka sasa kwenye Youtube ngoma ya Alikiba ya 'Seduce Me' imetazamwa na watu zaidi ya milioni 3, na Zilipendwa ya WCB imetazamwa na watu milioni 2.

No comments