Breaking News

Dkt. Kigwangalla atua Loliondo

Waziri wa maliasili na Utalii Dk. Hamisi Kigangwala amesema kuwa watoa huduma mbalimbali za utalii watatakiwa  kufuzu mtihani kabla ya kupewa leseni mpya kuanzia Januari 2018 ambapo Serikali itaandaa utaratibu mpya katika sekta hiyo.

Ambapo alisema kuwa Wizara yake iko katika mchakato wa kuandaa mwongozo kwa ajili ya makampuni ya utalii nchini pamoja na kufunga mashine maalumu ambayo itadhibiti mapato yatokanayo na utalii.

Aliongeza kuwa wizara yake itarekebisha mfumo wa watoa huduma katika sekta hiyo ambao umekuwa ukilalamikiwa na wadau mbalimbalui hasa watoa huduma za utalii wanaowashawishi watalii kutoka nchi mbalimbali za nje kuja kutembelea vivutio vya utalii vilivyoko nchini.

Dk. Kigangwala aliyasema hayo jana wakati alipokuwa anazungumza na watumishi wa Shirika la hifadhi la Taifa (Tanapa)katika ziara yake ya kutembelea ofisi mbalimbali za shirika hilo.

Alisema lengo hasa lakuanzisha mchakato huo utakaoanza kutumika mapema mwakani nikuweka vigezo vitakavyotolewa na Serikali kwa makampuni ili kuhakikisha wanakuwa na wahudumu watakaothibitishwa na wizara yake na kutoa cheti maalum kwa kila anaetoa huduma hiyo ya utalii.

Waziri huyo alisema lengo nikuboresha huduma za utalii ili kuwezesha upatikanaji bora wa huduma za utalii na mapato ambayo yanainua uchumi kwani Tanzania sasa inashindana na nchi mbalimbali katika kuvitangazavivutio vya utalii ili kuhakikisha watalii wenguwanakuja zaidi nchini kwetu.

Pia aliongeza kuwa watoa huduma za utalii wanapaswa kuzungumza vizuri kutoka nchi mbalimbali ili waweze kuja lakini pia waangalie jinsi ya kuboresha huduma za utalii ikiwemo mapatona mfumo huu mpya wa kukusanya mapatio ua sekta ya utalii kuboreshwa kuongeza mapato kwa mfumo wa kieletronik.

Aliongeza kuwa maeneo wanayoweka mkazo zaidi ni ukusanyaji wa mapato hiyvyo kutakuwa na dirisha moja litakalounganisha taasisi za utalii kujua mapato yanayoingia nikiasi gani na mtalii anakaa nchini kwa muda gani na hoteli ip na kujua mapato yamnayokusanywa kwa sekta ya utalii yanakuwa kwa kiasi gani.

Kwa upande wake Mkurugeni wa Tanapa Allan Kijazi alisema kuwa utaratibu huo utakuiwa mzuri na kpia wako katika mchakato wa kufungua ofifi katika mkoa wa dodoma ili kuweza kusogeza huduma mbalimbali zinazotoklewa nashirika huilo ili kuboresha sekta ya utalii na kuongeza pato la nchi kupitia sekta hiyo.

No comments