Breaking News

WANYARWANDA KUTOTAMBULIKA KAMA WAKIMBIZI

Mataifa mbalimbali duniani, hayatawatambua tena raia wa Rwanda waliokimbia nchi yao kati ya mwaka 1959 hadi 1988 kama wakimbizi baada ya muda waliopewa kurudi nyumbani kumalizika mwisho wa mwaka 2017.

Hatua hiyo inaamanisha kuwa, raia hao wa Rwanda hawatatambuliwa kama wakimbizi na hawatapa msaada wowote kutoka kwa Shirika la Umoja wa Mataifa linalowashughulikia wakimbizi UNHCR.

Disemba 31 mwaka jana, ilikubaliwa kati ya serikali ya Rwanda na Shirika la UNHCR pamoja na mataifa mbalimbali ambayo yamekuwa yakiwapa hifadhi wakimbizi hao kutoka Rwanda warejee nyumbani.

Mkataba wa kurejesha nyumbani wa wakimbizi uliokubaliwa mwaka 1951, unawataka wakimbizi kurejea katika nchi zao baada ya kubainika kuwa, hawapo tena katika hatari ya kushambuliwa au kunyanyaswa.

Wanyarwanda wanaoishi nje ya nchi yao ambao wamekuwa wakifahamika kama wakimbizi ni takriban elfu 20 kwa mujibu wa takwimu za Umoja wa Mataifa.

No comments