Breaking News

UMOJA WA MATAIIFA WAMTAKA RAIS KABILLA AJIUZULU

Umoja wa Mataifa umemwambia Rais wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo (DRC) Joseph Kabila kutimiza ahadi aliyoiweka ya kuachia madaraka na kupisha uongozi mwingine kuiongoza nchi hiyo hususani wakati huu ambapo nchi hiyo imejaa migomo na maandamano ya kushinikiza ajiuzulu.

Rais Kabila mwenye miaka 46, ameiongoza DRC kwa miaka 117 na msimu wake wa mwisho wa uongozi uliisha tangu December 31, 2016 na akatakiwa aachie ngazi lakini uchaguzi wa kupata Rais na viongoi wapya umekuwa ukiahirishwa mara kwa mara.

Suala hili limesababisha vurugu na maandamano ya raia wa DRC ambao hata hivyo inaelezwa kuwa wamekuwa wakipigwa na askari polisi jamabo ambalo kwenye taarifa ya Umoja wa Mataifa iliyotolewa December 31, 2017 imelaani vikali vitendo hivyo hususani Jijini Kinshasa ambapo watu watano waliuawa na polisi siku hiyo vya Jumapili kwenye maandamano.

No comments