Breaking News

Mbunge wa Mtwara Mjini (CUF), Maftaha Nachuma Akanusha Kuhamia CCM


Mbunge wa Mtwara Mjini (CUF), Maftaha Nachuma amewataka wananchi wa jimbo hilo kupuuza taarifa zinazosambaa kwamba ana mpango wa kujiondoa katika chama hicho.

Amesema anaendelea kuwatetea wakazi hao ili wapate maendeleo.

“CUF hawana historia ya kuhamahama vyama, hata huyo aliyeondoka ameondoka kwa masilahi binafsi. Mimi Maftaha Nachuma nitakuwa wa mwisho kuondoka CUF,” alisema jana Jumatano Desemba 6,2017.

Alisema suala la wabunge kujitoa katika nafasi zao linasababishwa na njaa kutokana na kuangalia masilahi binafsi bila kutetea wananchi.

Nachuma alisema wabunge wengi walidhani wakipata nyadhifa hizo watakuwa wananufaika kwa kupata fedha lakini sasa hilo halipo kwa kuwa ubunge siyo dili bali ni kwa ajili ya kuwatumia wananchi.

Kupitia mitandao ya kijamii imeelezwa kwamba mbunge huyo ana mpango wa kujiondoa CUF na kujiunga na CCM.

Nachuma alisema wanaosambaza taarifa hizo wana nia mbaya ya kumchafua kwa masilahi binafsi.

No comments