Breaking News

Diamond Atuhumiwa Kuwadhalilisha Wanawake.....Ni Baada ya Kumtaka Mtoto Wake wa Kiume Awatumie Atakavyo!

Msanii Diamond Platnumz anayetamba na Ngoma ya Sikomi ameingia matatani baada ya  watu mbalimbali kumtuhumu kuwadhalilisha wanawake kupitia ujumbe wake aliouandika katika ukurasa wake wa Instagram.

Ujumbe huo ambao ulikuwa ni maalum kwa ajili ya kumtakia heri ya kuzaliwa mtoto wake wa kiume, Nillan, ulimtaka mtoto huyo akue salama ili aje awatumie wanawake vyovyote atakavyo kwa sababu  anajituma ili amwandalie pesa ya kutumia vyovyote atakavyo atakapokuwa mkubwa.

“Nasemaje! Kua Uje kuwatembezea Baba... We swala la Kutafta ela niachie mie... Jukumu lako ni moja tu, Kupita nao.....Happy 1st Year Lanny!!!”Unasomekla ujumbe huo wa Diamond.

Ujumbe huo ulionekana kuwakera watu wengi hasa wanawake, ambao waliamua kumfungukia na kumpa makavu.

<< INGIA HAPA KUONEA   WANAWAKE WALIVYOMVAA DIAMOND>>

Visit website

No comments