Breaking News

MAVUGO AKALIA KUTI KAVU SIMBA

Viongozi wa Simba wameonyesha kutofurahishwa na uchezaji wa mshambuliaji wao Laudit Mavugo hasa kutokana na kushindwa kuonyesha juhudi uwanjani.

Habari za uhakika kutoka ndani ya Simba zimeeleza, viongozi wa Simba wamemtaka Mavugo kujituma na kama inashindikana basi wataachana nao.

"Viongozi hawajafurahishwa na Mavugo kwa kuwa hajaonyesha juhudi zozote katika mechi dhidi ya Simba.

"Unajua hata katika upangaji, awali kocha alionekana kama nafasi ya kuanza angempa Bocco. Lakini alibadili ikawa ni Mavugo," kilieleza chanzo.

"Viongozi wao hawana uwezo wa kumuingilia kocha lakini wanakerwa na namna Mavugo asivyoonyesha kama ana uchungu. Hivyo walitaka kama ameshindwa aende zake.

"Tayari kaelezwa kuwa lazima ajitume na acheze kuitumikia timu na kuisaidia kwa kuwa kama ilivyo kwa wengine anapata kila kinachotakiwa."

No comments