Breaking News

MEYA WA KINONDONI ANAKUPATAARIFA HII MUHIMU

HALMASHAURI ya Manispaa ya Kinondoni, jijini Dar es Slaam,  imeanza utekelezaji wa ujenzi wa  mradi  wa kiwanda cha mbolea chenye  kutumia malighafi ya taka  za kwenye masoko.

Zaidi ya   sh.bilioni 4.1 zinatarajiwa kutumika  katika awamu ya kwanza ya ujenzi wa kiwanda hicho kitakachojengwa katika eneo la Mabwepande.

Mradi huo  unajengwa kwa ushirikiano wa  wa Serikli ya Ujerumani kupitia jiji la  Humburg  na serikali ya Tanzania kupitia jiji la Dar es Saaam.

Kata makubaliano  kati ya majiji la  haya mawili  Jiji la Humburg  litaghramia  ujenzi  wa mradi huo  na kuuendesha kwa muda wa mwaka mmoja  ambapo  itahusika pia  katika kujenga  uwezo wa wataalamu  wa manispaa katika uendeshaji wa kiwanda.

Akizungumza  wakati wa kikao cha wadau  wa mradi huo, Dar es Salaam, jana, Mstahiki Meya wa Halmashauri ya Manispaa ya Kinondoni, Benjamin Sitta, alisema  jiji la Humburug litatoa  sh.bilioni 2.78 na  sh.bilioni 1.32 zitatolewa na serikali kuu ya Ujerumani.

‘’ Chini ya makubaliano hayo Msanispaa ya Kinononi  itagharamia upatikanaji wa  kiwanda  na tayari ekari 14 zimepatikana.Pia Manispaa itagharamia miundombinu  ya barabara, maji na umeme kiwandani,’’alisema Meya Sitta.

Aliongeza: ‘’Ujenzi wa kiwanda  hicho  unatarajiwa  kuanza  mapema mwezi  huu na taratibu za ununuzi  na kumpat  mkandarasi wa ujenzi  zipo katika hatua za mwisho.Ujenzi utachukua miezi 12,’’

Alisema  radi huo utakapokamilika utakuwa na faida nyingi ikiwa ni pamoja na kupunguza taka za kwwenye masoko .

‘’Wastani   wa tani 180  za taka huzalishwa kila siku  katika masoko yaliypo ndani ya Manispaa ya Kinondoni na uwezo wa  wa kiwanda ni  kuchakta taka   tani 50 kwa siku .Kiwanda kitakuwa na uwezo wa kuzalisha tani 25 za mbolea kwa siku,’’alieleza Meya huyo.

Alitaja faida zingine kuwa ni kuongeza  mapato ya Manispaa kutokana na mauzo ya mbolea, kupunguza matumizi ya mbolea zenye  kuleta athari kwenye ardhi  na afya za binadamu pamoja na kuongeza fursa za ajira kwa watanzania.

Alisema  utekelezaji wa mradi huo awali ulisimama kutokana na Manispaa hiyo kusaini mkataba wa utekelezaji  moja kwa moja na jiji la Humburug, hali ambayo kiutaratibu ilifanya serikali kushindwa  kuondoa  kodi.

Kwa upande wa Mwakilishi wa Jiji la Humburg  Dk. Florian Koelch  alisema,  kiwanda hicho kitajengwa   katika eneo la heka mbili litakalosakafiwa na litahifadi taka  kwaajili  ya kuozeshwa  ambalo litakuwa salama  kwa unyevu

‘’Hatua hii ya mwanzo huchukua wiki mbili  na baada ya hapo taka  zisizooza  huhamishiwa  sehemu maalumu. Mchakato wa uozeshaji taka  huchkuaa  wiki nane hadi 10. Mradi huu utasajiliwa kama mradi wa kulinda  mazingira chini ya  ya tasisi ya The gold standard –GS’’ alisema Koelch.

Mradi huo utasimamiwa na  kampuni ya Atmosfair ya nchini Ujerumani.

No comments