Breaking News

Antonio Conte anaondoka Chelsea?

Italy's coach Antonio Conte looks on during the Euro 2016 group H qualifying football match between Italy and Malta on September 3, 2015 at the Artemio Franchi stadium in Florence. AFP PHOTO / ALBERTO PIZZOLI (Photo credit should read ALBERTO PIZZOLI/AFP/Getty Images)

Hakika msimu uliopita ulikuwa bora sana kwake kwani aliifanya Chelsea kucheza vizuri sana na katika msimu wake wa kwanza tu na klabu hiyo ya Uingereza kocha huyo alifanikiwa kutwaa kikombe cha ligi ya Epl.

Baada ya ligi kuisha mambo yanaonekana sio mazuri kwake kwani watu wake wa karibu wamekuwa wakidai Antonio Conte hana furaha Uingereza haswa kutokana na vyombo vya habari vinavyomuandika kocha huyo.

Wiki za karibuni kocha huyo amekuwa akiandikwa sana katika vichwa vya habari vya magazeti na mitandao mbalimbali baada ya kuibuka tuhuma za kumtumia Diego Costa ujumbe mfupi kwenye simu akimuambia hamtaki.

Inafahamika kwamba tangu Conte akiwa nchini Italia anapenda maisha ya kutotokea sana katika vyombo vya habari lakini hali inayotokea Uingereza inamsumbua sana kichwa na imekuwa ikimkosesha raha.

Lakini pia taarifa zinadai mmiliki wa klabu ya Chelsea Roman Abromovich umekuwa tatizo sasa na ndio sababu hadi sasa Chelsea hawajasajili kwani tajiri pesa aliyotoa ya usajili ni ndogo kuweza kununua wachezaji wakubwa.

Antonio Conte ana ndoto za kubeba kombe kubwa la Champions League lakini tayari ameona bajeti ndogo ya usajili aliyopewa inaweza kuwa kikwazo kwake kuchukua kombe hilo na hii imemfanya kukosa raha.

Ripoti zinasema Conte sasa amechukia zaidi kwani amekuwa akiahidiwa tu kuhusu kununua wachezaji lakini pesa hapewi na sasa anataka kuonana moja kwa moja na Roman Abromovich au Marina Granovaskia ambae ni kati ya wafanya waamuzi wakuu wa Chelsea.

Conte pia anakosa raha kutokana na kukosa control ya academy ya soka ya Chelsea na mambo yote hayo yanamfanya kuanza kuwaza kuondoka lakini bado kuna nafasi kubwa ya kubaki kwani Roman anafuatilia kwa karibu kutaka kununua majina makubwa ikiwemo Lukaku na Morata.

No comments