Singida United yatumia busara za Mwl. Nyerere

Akiongea
na East Africa Television Sanga amesema kuwa wao kama timu
hawkauangalia sana mkataba unasema nini kwani mchezaji naye ni binadamu
na ana maisha nje ya soka.
''Ni kweli tulimruhusu mlinzi wetu na timu ya taifa ya Zimbambwe
Elisha Muroiwa kwenda kushughulikia matatizo ya kifamilia tangu Disemba
mwaka jana lakini sasa amerejea, tulitumia busara tu na hata Nyerere
alisema sheria ikitumika sana tutashindwa kuendesha nchi'', - amesema.
Sanga pia ameongeza kuwa kipindi chote ambacho Muroiwa alikuwa kwao,
walihakikisha anaendelea na mazoezi kwenye klabu ya Harare City Stars
ambayo walimkabidhi ili asipoteze kiwango.
Muroiwa tayari amerejea nchini na ameshajiunga na timu hiyo ambayo
ipo jijini Arusha tayari kwa maandalizi ya mchezo wa fainali ya Kombe la
FA.
No comments