Breaking News

Mbaroni kwa kuweka mwili wa mama yake kwenye jokofu

Polisi nchini India wameeleza kuwa wanamshikilia mwanaume mmoja ambaye aliweka mwili wa mama yake mzazi aliyekufa kwenye freezer na kuishi nao kwa miaka 3.

Mtuhumiwa huyo Subhabrata Majumdar anaelezwa kuwa aliweza kutunza mwili huo kwenye freezer kwa kutumia kemikali za kuuchoma mwili wa marehemu.

Uchunguzi juu ya tukio hili unaendelea huku polisi wakieleza kuwa wanahisi alitunza mwili huo ili apate mafao ya mama yake na pia alikuwa akiamini kuwa mama yake atazaliwa upya kama mwili wake utatunzwa.

No comments