Breaking News

MAMLAKA YA HALI YA HEWA YATOA TAHADHARI

Mamlaka ya hali ya hewa iliyopo chini ya Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano nchini Tanzania imewatahadharisha wananchi kuwepo kwa hali mbaya ya hewa katika maeneo ya mikoa ya Dar es Salaam, Pwani, Lindi na Mtwara ndani ya saa 24 kuanzia leo.

Hayo yamebainishwa na taarifa zilizotolewa na mamlaka hiyo na kudai kutakuwepo vipindi vifupi vya mvua kubwa ambazo zinatarajiwa kunyesha katika baadhi ya maeneo ya mikoa ya Singida, Dodoma, Morogoro, Ruvuma, Njombe, Iringa, Mbeya, Songwe, Kilimanjaro, Manyara na Arusha

Mbali na hilo, TMA imesema kutakuwepo upepo mkali unaofikia kilomita 30 kwa saa kutoka Kaskazini- Mashariki kwa Pwani ya Kaskazini na kutokaa Kaskazini-Magharibi kwa Pwani ya Kusini huku hali ya bahariinatarajiwa kuwa na mawimbi makubwa kiasi.

No comments