Breaking News

TANZANIA NA MSUMBIJI KUBADILIHSANA UZOEFU WA GESI NA MAFUTA


Rais wa Jamhuri ya Msumbiji MheFilipeJacinto Nyusi amefanya ziara ya kikazi yasiku moja hapa nchini ambapo amekutana nakufanya mazungumzo na Rais wa Jamhuri yaMuungano wa Tanzania MheDkt. John Pombe Magufuli Mjini Dodoma.

MheFilipe Jacinto Nyusi amepokelewakatika uwanja wa ndege wa Dodoma namwenyeji wake MheRais Magufulialiyeongozana na Makamu wa Rais Mhe.Samia Suluhu Hassan na Waziri Mkuu Mhe.Kassim Majaliwa Majaliwa na kisha viongozihao wamefanya mazungumzo rasmi nakusalimu wananchi kupitia vyombo vyahabari.

MheRais Nyusi amemshukuru MheRaisMagufuli kwa kumpokea na kufanya naemazungumzo na amesema ujio wakeumelenga kuimarisha na kukuza zaidiuhusiano na ushirikiano wa kihistoria nakidugu kati ya nchi yake na Tanzania.

“MheRais Magufuli japo kuwa nimetoataarifa ya muda mfupi kuwa nakuja kuonananaweumenikaribisha umenipokea natumezungumza mambo yenye manufaa kwanchi zetunakushukuru sana” amesema Mhe.Rais Nyusi.

Amebainisha kuwa yeye na Rais Magufuliwamezungumzia namna Tanzania naMsumbiji zitakavyobadilishana uzoefukuhusu ugunduzi mkubwa wa gesi na mafutauliofanikiwa katika nchi hizimasuala yaulinzi na usalama na uimarishaji wamiundombinu ya usafiri.

Kwa upande wake MheRais Magufuliamemshukuru MheRais Nyusi kwa kujaMjini Dodoma na kwa kudumisha uhusiano naushirikiano wa kidugu na kihistoriauliojengwa na waasisi wa mataifa haya HayatiBaba wa Taifa Mwl. Julius KambarageNyerere na Hayati Samora Machel waMsumbiji.

MheRais Magufuli amesema katikamazungumzo hayo pia wamekubaliana Tumeya pamoja ya ushirikiano ya Tanzania naMsumbiji zikutane haraka ili kuimarishamaeneo yote ya ushirikiano kwa manufaa yanchi hizo.

“Nafurahi kuwa MheRais Nyusi piaamesema Msumbiji itatoa kibali kwa Shirikala Ndege la Tanzania (ATCLkufanya safari za moja kwa moja kati ya Tanzania naMsumbiji haraka iwezekanavyo, ili kurahisisha usafiri kati yetu” amesisitiza Mhe. Rais Magufuli.

Mhe. Rais Nyusi ameondoka nchini jana jioni  na kurejea nchini Msumbiji.

 

Gerson Msigwa

Mkurugenzi wa Mawasiliano ya Rais, IKULU

Dodoma

No comments