Breaking News

MANENO YA HAJI MANARA BAADA YA KILIMANJARO STARS KUFUNGWA "TUMEROGWA NA NANI?

Timu ya taifa ya Tanzania bara maarufu kama Kilimanjaro Stars iliyopo nchini Kenya katika michuano ya Kombe la CECAFA Senior Challenge Cup leo imecheza mchezo wake wa kukamilisha ratiba wa michuano hiyo dhidi ya timu ya taifa ya Kenya ambao ndio wenyeji wa michuano hiyo.

Kilimanjaro Stars leo imepoteza kwa goli 1-0 dhidi ya Kenya ikiwa ni mchezo wake wa tatu kupoteza wa hatua ya makundi katika michezo yake minne ikiwa imeambulia sare mchezo mmoja dhidi ya Libya katika mchezo wao wa kwanza.

Afisa habari wa Simba Haji Manara ni miongoni mwa watanzania ambao hawajafurahishwa na matokeo na perfomence ya Kilimanjaro iliyoionesha katika michuano ya Challenge msimu huu na katika ukurasa wake wa instagram akaamua kuandika hivi.

“Why always us?tumerogwa na nani?wapi tunakosea kama nchi?hatuna talents au programs?nn tufanye ili tuepuke fedheha hz?Serikali, TFF vilabu na wadau wote lazma tutafute suluhisho la aibu hii @harrisonmwakyembe @tanfootball @azamtvtz”>>> Haji Manara

No comments