Breaking News

BINADAMU MWENYE TATOO NYINGI ZAIDI DUNIANI

Mwanaume mmoja raia wa Uingereza Paul Allen anasemekana kuwa ndiye binadamu mwenye tattoo nyingi kuliko mtu yeyote dunia ambazo kwa sasa ziko 812 katika kila sehemu ya mwili wake hadi sehemu za siri na sehemu pekee kwenye mwili wake isiyo na tatuu ni ndani ya macho tu.

Ameeleza kuwa alianza kujichora tattoo hizo akiwa na umri wa miak 49 wiki moja baada ya mama yake mzazi kufariki na tangu hapo hajawahi tena kuacha wala kuridhika na wingi wa tattoo hizo zilizo mwilini mwake.

Ameongezea pia kuwa hadi sasa ametumia zaidi ya Euro 15, 000 (Takriban Tsh 40 milioni) kama gharama ya kuchora tattoo hizo.

No comments