Breaking News

TAKUKURU imekamilisha upelelezi kesi ya Aveva, Jalada bado lipo kwa DPP

Upande wa mashtaka umeieleza Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu kuwa jalada la kesi ya utakatishaji fedha na kugushi inayomkabili Rais wa Simba SC, Evans Aveva na Makamu wake Geofrey Nyange Kaburu, lipo kwa DPP baada ya TAKUKURU kumaliza upelelezi.
Mwendesha mashtaka wa TAKUKURU, Leornad Swai amemueleza Hakimu Mkazi Mkuu, Victoria Nongwa kuwa kesi hiyo imeitishwa kwa ajili ya kutajwa na jalada lipo kwa DPP, ambapo wanasubiri majibu yake ili kuona kama upelelezi umekidhi matakwa ya kisheria.
Baada ya kuelezwa hayo, kesi imeahirishwa hadi October 25, 2017.

No comments