Breaking News

#NEWS Mahakama yamuachia huru Manji

Upande wa utetezi ulikuwa na mashahidi saba na wa mashtaka ulikuwa na mashahidi watatu.

Dar es Salaam. Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu, imemuachia huru mfanyabiashara Yusuph Manji(41) baada ya upande wa mashtaka kushindwa kudhibitisha shtaka dhidi yake.

Mahakama ya Hakimu  Mkazi Kisutu leo imetoa hukumu katika kesi ya kutumia dawa za kulevya iliyokuwa ikimakabili Manji.

Hukumu hiyo imetolewa leo Ijumaa na Hakimu Mkazi Mfawidhi wa Mahakama hiyo, Cyprian Mkeha baada ya upande wa mashtaka na wa utetezi kufunga ushahidi.

Katika kesi hiyo, upande wa utetezi ulikuwa na mashahidi saba na wa mashtaka kuwa na mashahidi watatu.

Awali, Manji kupitia wakili wake Hajra Mungula aliieleza Mahakama kwamba angekuwa na mashahidi 15.

Katika kesi hiyo, Manji anadaiwa kati ya Februari 6 na 9, eneo la Sea View, Upanga wilayani Ilala alitumia dawa za kulevya aina ya heroin.

Ushahidi wa upande wa utetezi  mahakamani unaonyesha Manji ana vyuma kwenye moyo.

Mfanyabiashara huyo katika utetezi wake  alidai ana matatizo ya moyo ya kurithi kutoka kwa babu zake na alianza kuugua akiwa na miaka 26.

No comments