MTIBWA SUGAR KUVAANA NA YANGA JUMAMOSI
Klabu ya Mtibwa Sugar kutoka Turiani mkoani Morogoro inataraji kutinga uwanjani siku ya Jumamosi tarehe 30.09.2017 kucheza mchezo wa ligi kuu bara namba 34 dhidi ya Young Africans utakaopigwa katika uwanja wa Uhuru jijini Dar es laam.
Klabu ya Mtibwa inayomilikiwa na kiwanda cha kuzalisha sukari bora nchini Mtibwa Sugar ni klabu inayo ongoza msimamo wa ligi kuu bara hadi sasa kwa kwa kufanikisha kukusanya pointi 10 katika michezo 4 iliyocheza kwa upande wa Young Africans wao wanashika nafasi ya 6 baada ya kukusanya pointi 8 katika michezo 4 ya ligi kuu bara.
Mchezo huo unatarajiwa kuwa mkali kutokana na matokeo ya timu hizi mbili karibuni kuwa mazuri ila Mtibwa Sugarikionekana bora na kuongoza ligi kuu bara hadi mzunguko wa nne.
Kuelekea mchezo huo kikosi cha wana tam tam kimejichimbia mkoani Morogoro katika maskani yake Madizini Turiani kikiendelea na maandalizi ya mchezo huo wa Jumamosi.
Mchezo wa mwisho baina ya timu mbili zilitoka sare ya bila kufungana katika uwanja wa Jamhuri mkoani Morogoro na Jumamosi zitakutana katika uwanja wa Uhuru .
RATIBA:
MCHEZO: Young Africans V Mtibwa Sugar
LEAGUE: Vodacom Premier League
SIKU: Jumamosi
TAREHE: 30.09.2017
UWANJA: Uhuru Stadium
No comments