Breaking News

Wakenya waanza kumiminika Tanzania

Hofu imetawala kina kona nchini humo wakati siku za uchaguzi mkuu zikikaribia

 Joto la uchaguzi wa nchini Kenya limezidi kupamba moto kufuatia

idadi ya Wakenya wanaoingia Tanzania kwa kuhofia fujo ikizidi kuongezeka.

Mwananchi ilikuwa katika vijiji vilivyo jirani na mpaka wa

Horohoro mkoani Tanga na kukuta idadi ya wanaovuka kutoka Kenya

kuingia Tanzania kuwa  kubwa ikilinganishwa na siku ambazo si za

uchaguzi.

Mwanakombo Ali ambaye ni Mkazi wa Vanga nchini Kenya amesema

amelazimika kuondoka kutokana na hofu kwamba

huenda siku ya uchaguzi ikatokea vurugu.

“Mimi na watoto wangu watatu tumekuja hapa Duga Maforoni kwa baba

yangu,huku ndiko nyumbani kwetu na Vanga ni kwa mume wangu kwani hivyo

nimeona nising’anganie kukaa mahala ambapo tunaweza kuuawa ikitokea

vurugu”amesema Mwanakombo.

Salehe Mohamed amesema katika kijiji cha

Mwakijembe wilayani Mkinga mkoani Tanga kuwa yeye ni mkazi wa Mombasa

nchini Kenya na alikuwa amejiandikisha kupiga kura lakini kutokana na

hofu ya kutokea vurugu ameamua kuondoka yeye na familia yake ili

kuokoa maisha.

“Tutakaa hapa hadi uchaguzi utakapofanyika na kutajwa mshindi kwani

hali si shwari kwa sasa hivi akishinda Uhuru kutatokea vurugu na hata

akishinda Odinga kutatokea vurugu tu”amesema Salehe.

Katika mapaka wa Kenya na Tanzania,Mwananchi ilishuhudia abiria

wanaoingia Tanzania kupitia mabasi ni kubwa kuliko wanaokwenda Kenya

ambapo wengi wao ni raia wa wa Kiasia na kutoka nchi za Ulaya.

Ofisa mmoja idara ya uhamiaji katika ofisi ya Horohoro ambaye hakutaka

jina lake litajwe amesema kumekuwa na idadi kubwa ya abira wanaopita

katika mpaka huo wakitokea nchini Kenya kuingia Tanzania na sababu ni

kutokana na uchaguzi

No comments