Breaking News

Mnyate Abaki Simba Kibishi.


WINGA Jamal Mnyate aliyekosa nafasi katika kikosi cha kwanza cha Simba amefunguka na kusema kuwa bado ataendelea kuwemo katika klabu hiyo kutokana na kuwa na mkataba na timu hiyo.

Mnyate alisajiliwa na Simba akitokea katika klabu ya Mwadui kwa mkataba wa miaka miwili lakini tangu alivyosajiliwa alifanikiwa kucheza mechi kadhaa kutokana na mara nyingi akiwa anasumbuliwa na majeruhi.

“Kwa hivi sasa ni ngumu kusema msimu ujao nitakuwa wapi, kwasababu bado nina mkataba wa mwaka mmoja na Simba kikubwa mimi na wasikiliza wao waajiri wangu watakavyonambia kuhusu hatima yangu,”alisema.

Mnyate alisema hawezi kuzungumza chochote kwa sasa kutokana na kuwa bado yupo chini ya mkataba na timu hiyo, lakini angekuwa ameshamaliza nao mkataba angekuwa huru kusema msimu ujao angeenda timu gani.

Aidha,Mnyate amewapongeza  Viongozi wake kwa usajili walioufanya kwa kuwarudisha  wachezaji wao wa Zamani kama Emmanuel Okwi,Shomary Kapombe ambao walikuwa tishio  ligi kuu.

No comments