Breaking News

ALVARO MORATA AWAUA MAN UNITED


Manchester United wameendeleza rekodi mbovu dhidi ya timu kubwa baada ya hii leo Jose Mourinho kupoteza mchezo wake wa kwanza dhidi ya mabingwa watetezi.

Alikuwa Alvaro Morata dakika ya 55 kufunga bao pekee katika mchezo wa leo huku likiwa bao lake la nne la kichwa kati ya mabao saba aliyofunga msimu huu wa ligi.

Bao la leo la Alvaro Morata linamfanya mchezaji ambaye amefunga mabao mengi ya kichwa (10) kuliko mchezaji yoyote katika ligi kubwa tano barani Ulaya.

Matokeo ya leo yanawafanya Manchester City kuongoza ligi kwa tofauti ya alama 8 huku Chelsea wakipunguza pengo la alama na United na sasa wanatofautiana kwa pointi moja.

Katika matokeo mengine Everton waliokuwa nyumbani walitoka nyuma ya mabao mawili na kuibuka na ushindi wa mabao matatu kwa mawili dhidi ya Watford.

Watford  walitangulia kupata mabao mawili kupitia kwa Ricahrlison na Kabasele kabla ya Oumar Niesse na Lewin kuisawazishia Everton kisha Leighton Baines kufunga bao la ushindi.

Hii ni mara ya kwanza kwa Everton kutoka nyuma kwa mabao mawili na kuibuka na ushindi tangu wafanye hivyo mara ya mwisho mwaka 1994 dhidi ya Wimblendon Memories.


No comments